DHAMIRA YA BINADAMU KUTENDA WEMA KATIKA DIWANI YA MASHAIRI YA SAADANI
Keywords:
Maana za kimaadili, uwakilishi wa wema, diskosi ya kishairi ya Kiswahili, maadili ya kibinadamu, Diwani ya Mashairi ya Saadani ya Saadani Abdu KandoroAbstract
Makala haya yanahusu kuchunguza dhamira ya binadamu kutenda wema katika diwani ya Mashairi ya Saadani iliyoandikwa na Saadan Abdu Kandoro mwaka 1972. Data za makala haya zimekusanywa kwa kutumia mbinu ya usomaji makini ambapo walisoma kwa makini diwani ya Mashairi ya Saadani kwa kuzingatia lengo la makala na kuweza kupata data za utafiti. Baada ya kukusanya data hizo za utafiti zilichambuliwa kwa kutumia mbinu ya kimaelezo. Makala yanaonesha kwamba katika diwani ya Mashairi ya Saadani kunawasilishwa dhamira ya kutenda wema ambapo binadamu anasisitizwa kutenda wema hata kwa watu ambao wamemfanyia ubaya kupitia mashairi mawili. Hakika huu ni msisitizo adhimu wa kuonesha umuhimu wa dhamira hii katika jamii.










