USAWIRI CHANYA WA MWANAMKE KATIKA NYIMBO TEULE ZA TAARAB ZA BAKARI ABEID
Keywords:
Usawiri, Kiumbe, Chanya, Nyimbo, dhanaAbstract
Makala haya yanahusu usawiri chanya wa mwanamke katika nyimbo za taarab za Bakari Abeid. Lengo kuu la makala lilikuwa ni kutaka kuchunguza namna mwanamke anavyosawiriwa katika hali chanya katika nyimbo za taarab za msanii maarufu za nyimbo za taarab anayefahamika kwa jina la Bakari Abeid. Makala yalikusanya data kwa kutumia mbinu ya usomaji makini na kuchambuliwa kwa kutumia mbinu ya kimaelezo na nadharia ya Ufeministi. Usawiri chanya wa mwanamke katika nyimbo za taarab za Bakari Abeid umejitokeza katika maeneo ya mwanamke kiumbe mwenye umbo zuri, mwanamke kiumbe mwenye msimamo, mwanamke kiumbe mwenye mapenzi ya kweli na mwanamke ni mtunza siri.










